Thursday, 28 December 2017

USHAHIDI KIAKIOLOJIA YA KUZUNGUMZWA KISWAHILI KABLAYA UJIO WA WAGENI KATIKA UPWA A.MASHARIKI

      Ushahidi wa Akiolojia ni mbinu wanazotumia wanahistoria kuchunguza Tamaduni za watu katika vipindi tafauti vya historia kwa kuchunguza mabaki ya majengo na vitu mbalimbali katika ardhi.
     Wanakiakiolojia wanatafuta vitu vilivyobaki katika Ardhi  kwa mfano mabaki ya majengo,silaha,mbegu,vyombo,makaburi na mifupa ya watu.
      Ushahidi  wa  kiakiolojia  unathibitisha wazi kuzungumzwa kwa  Kiswahili  kabla  ya  kuja kwa  wageni  katika  mwambao wa Afrika ya mashariki kama ifuatavyo:
     Kugunduliwa kwa  miba  ya samaki, ushahidi huu unaonesha kuwa wakaazi wa  mwambao wa  Afrika ya mashariki kama  vile  Lamu,Kilwa walikuwa wakijishughulisha na shughuli za uvuvi, hivyo katika harakati zao  waliweza  kuwasiliana kwa kutumia lugha ya Kiswahili.  Ushahidi  wa hili   tunauona baada ya NEVILLE CHITTICK kufanya ugunduzi mwaka 800BK -1100BK.
     Kugunduliwa kwa vyungu vya kienyeji,kabla ya kuja kwa wageni Waswahili wa Mwambao, wa Afrika ya mashariki walijishughulisha na kazi ya kufinyanga vyungu ambavyo kwa wakati huo vilikuwa having’arishwi,hivyo kugunduliwa kwa mabaki ya vyungu katika mijiya Manda,Shanga Kilwa ambayo vilitumika katika miaka ya 800 hadi 1000 hivi vinaonesha kuwa kazi hii ilikuwa ni ya utamaduni wa waswahili,hivyo hata  lugha waliyokuwa wakiizungumza ni ya Kiswahili, hivyo inathibitisha kuwa Kiswahili kilitumika hata kabla ya kuja kwa wageni.
      Kugunduliwa kwa mashimo ya majengo,historia inatueleza kwamba kabla ya kuja kwa wageni katika mwambao wa Afrika ya mashariki,Waswahili waliishi katika nyumba zilizojengwa kwa miti nakukandikwa kwa udongo kama ni moja ya sehemu ya utamaduni wao,hivyo ushahidi wa kimachimbo uliofanywa na MARK KARTON katika mwaka 920-1020 amegunduwa mashimo yaliyokaa duara na mengine yaliyokaa mstatili kuashiria kwamba hapo awali Waswahili wa mwambao walijenga nyumba za miti na lugha iliyotumika ni Kiswahili.
       Kugunduliwa kwa shanga za simbi,vilevile kugunduliwa kwa shanga za simbi katika mwambao wa Afrika ya mashariki mfano katika maeneo ya Manda na Kilwa mnamo mwaka 800-1000 kunaonesha wazi kuwa Waswahili wa kimwambao walijishughulisha na utengenezaji wa shanga za simbi ambazo zilikuwa kama ni mapambo yao na hivyo kwasababu ya Utamaduni wao kuwa ndio huo basi na  lugha yao ikawa ni Kiswahili.
      Kugunduliwa kwa chuma, pia katika ushahidi wa Akiolojia uliofanywa na CHITTECK unabainisha wazi kuwa waswahili waliweza kugunduwa makapi ya chuma na wakaweza kuyeyusha na kufua chuma na kutengeneza Ndoana,vichwa vya Mishare na, hata Majembe na Shoka, hivyo vitu hivi ndiyo walivyovitumia katika maisha yao ya  kila siku, ambapo pia wanaashiria hata lugha waliyokuwa  wakizungumza ni Kiswahili.
       Kugunduliwa kwa Mbegu za Mtama ,ushahidi huu unaonesha kwamba waswahili wa mwambao wa Afrika ya mashariki walikuwa  wakijishughulisha na ukulima na hasa kilimo cha Mtama, na inaonesha kuwa waswahili huwo ulikuwa ndio utamaduni wao wa Kiswahili na hata lugha yao ikawa ni ya Kiswahili. CHITTECK anasema “Nao walikuwa wakulima katika wakati huo’’.
         Pia MARK KARTON ametenganisha vipindi 5 katika ukuwaji wa mji wa Shanga:
         850-920 safu hii ilionesha mabaki ya vyungu, mbeguza mtama, katika safu hii nyumba havikuwa bayana.
        920-1020  safu hii inaonesha majengo yaliyokaa duara na juu yake yapo ya mstatili yaliyokandikwa kwa udongo na kushikiliwa kwa fito.
       1020-1250 safu hii inaonesha matumizi ya matumbawe kushikiliwa kwa udongo katika msingi kisha pakajengwa nyumba ya miti iliyochanganywa na fito na kukandikwa kwa dongo.
          1250- 1320         Safu hii inaonesha chokaa ilitumika kujenga msikiti mzuri zaidi na paa lililojegwa kwa kutumia mbao.
          1320-1440 safu hii ilionesha matumizi ya paa za sleti, matumbawe,chokaa na mchanga zilitumika katika ujenzi wa nyumba.
        Kwa kupitia safu hizi kwa vipindi tafauti, pia inaonesha jinsi waswahili wa mwambao walivyokuwa na utamaduni wao wa  makaazi  na jinsi walivyokuwa na utaalamu wa kusanifu makazi yao,na hii inaonesha hata lugha yao ya mawasiliano ni Kiswahili kwa wakati huo.
       Hivyo basi ushahidi wa Kiakiolojia nao unatusaidia katika kutupatia mfuatano bayana wa tarehe kuhusu maendeleo ya awali ya watu waliokuwa wanazungumza Kiswahili katika mwambao wa Afrika ya mashariki hata kabla ya kuja kwa wageni.
                    














waswahili wa pwani


MASHAIRI YA PWANI


RAMANI YA MWAMBAO WA AFRIKA YA MASHARIKI


MAENDELEO YA KISWAHILI KATIKA ELIMU NA MAWASILIANO

Lado (1064), Lugha ni chombo cha mawasiliano baina ya binaadamu katika jumuiya fulani. Potta (1960), Lugha ninutaratibu wa alama za sauti zilizopangiliwa kutokana na mazoea au matamshi ya watu kwa njia ya sauti, ambazo wanaadamu wanapelekeana habari na wanasikilizana. TUKI(2004), Lugha ni mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wataifa au kundi Fulani kwa ajili ya kuwasiliana. Lugha ya Kiswahili ni lugha ambayo inatumiwa na watu wenye utamaduni na asili ya upwa wa pwani ya Afrika Mashariki katika shughulizao za kila siku. Hivyo kutokana na kunea na maendeleo ya Kiswahili, sasa inaonekana lugha ya Kiswahili kuwa na watumiaji wengi zaidi ndani na nje ya Afrika Mashariki, kupelekea lugha hii ya Kiswahili kupata nafasi ya tano kutoka ya saba katika lugha bora za Ulimwenguni. Hata hivyo,kutokana na hatua hii kubwa ya lugha ya Kiswahili, tayari kimekwishakubaliwa katika matumizi mbalimbali yakiwemo ya kielimu na kimawasiliano nje ya Afrika Mashariki. Kwa kuanzia na mafanikio ya lugha ya Kiswahili katika elimu kama ifuatavyo:- Kuanzishwa kwa vyuo mbali mbali ambavyo vinafundisha lugha ya Kiswahili. Kiswahili kimefanikiwa duniani kupitia harakati mbalimbali za elimu ambapo Kiswahili kimepata fursa ya kufundishwa katika vyuo mbalimbali,ikiwemo marekani amboyo inaongoza kwa kuwa na vyou vikuu 50 ambavyo vinafundisha lugha hii ya Kiswahili.Mfano wa vyuo hivyo ni Harverd Universuty, Massachusetts Institute of Technology, Starnford University, University of Oxford na University of Cambradge ambavyo vinapatikana Marekani na Uingereza. Pia, kuundwa kwa idara mbalimbali ambazo zinazoshughulikia zaidi ukuzaji na matumizi ya Kiswahili.Nje ya Afrika Mshariki lugha ya Kiswahili imefanikiwa kielimu kwa kuanzishwa kwa taasisi na idara nyingi ambazo zimepewa jukumu la kushughulikia ukuzaji na matumizi ya Kiswahili. Miongoni mwa idara hizo ni idara ya lugha na fasihi za kiafrika katika chuo kikuu cha Wistonsin U.S.A,idara ya masomo ya kiafrika kozi ya sanaa na sayansi ya jamii katika chuo kikuu cha Brunswikk U.S.A, Taasisi ya masomo ya lugha na utamaduni wa Ulaya na Afrika- Japan na Idara ya Kiswahili katika chuo kikuu cha masomo ya kigeni Haunkuk-Korea. Vilevile, Kiswahili kimekwisha kubaliwa kutumika katika shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia elimu,sayansi na utamaduni. Lugha ya Kiswahili kimefanikiwa nje ya Afrika Mashariki katika elimu, kwa kukubalika matumizi ya lugha Kiswahili katika shirika hilo la umoja wa mataifa ambalo ni chombo muhimu sana katika elimu ambacho ni UNESCO. Kuengezeka kwa watu kutoka mataifa mbalimbali.Watu kutoka mataifa mbalimbali ya Ulaya,Amerika na Asia kuja Afrika Mashariki kwa ajlil ya kujifunza lugha ya Kiswahili na kufanya tafiti mbalimbali zinohusiana na lugha ya Kiswahili ikwa ni moja ya mafanikio ya lugha ya Kiswahili. Tukiachana na mafanikio haya ya kielimu pia kwa upandewa kimawasilino kuna mafanikio kadhaa ya lugha ya Kiswahilikama vile:- Kwa upande wa maendeleo ya mtandao wa Intaneti .Kwa kiasi kikubwa imefanikisha juhudi za kukuza na kueneza Kiswahili duniani, hasa kupitia matumizi mbalimbali katika mtandao huo,wataalamu,wanasiasa na pamoja na watu mbalimblia wanatumia muda mwingi katika kuwasiliana, kutoa habari na hata kujifuna mengi katika mtandao kupitia progranu mtandaoni, katika injini pekuzi na kwabahati njema harakati zote hizo kwa sasa tunazipata kwa 100% kupitia lugha ya Kiswahili. Jambo ambalo hupelekea watu wengi kutumia chombo hicho kwa wakati mmoja na kuzidi kutumia mawanda ya utumizi wa lugha ya Kiswahili duniani kote.kwa mfano kupitia google injin unaweza ukasachi kwa kutumia lugha ya Kiswahili. Pamoja na hayo, matumizi ya lugha ya Kiswahili katika vyombo vya habari kama vile redio, runinga na magazeti yamaendelea kuipa nguvu lugha ya Kiswahili. Hasa kwa kuongeza mara dufu vituo vya kutolea habari ambapo kupitia redio mbalimbali za kimataifa, zimekuwa zikitoa habari na matangazo yake katika lugha ya Kiswahili.Kwamfano wa vyombo vya habari hivyo ni sauti ya Amerika,shirika la utangazaji la Uingereza (BBC), sauti ya Ujerumani (DW), idhaa ya Kiswahili ya china na hata idhaa ya Kiswahili ya Jamuhuri ya Kiislamu ya Iran. Ambapo Kiswahili kimefikia kiwango cha juu kabisa cha kusikika , kwani sasa vinasikika dunia nzima. Ama kwa upande wa Magazeti nayo pia yanachukua nafasi kubwa katika kuunga mkono juhudi za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili duniani, ambapo magazeti mbali mbali hasa ya Ujerumani yanaelezwa kwa Kiswahili na baadhi ya magazeti hayo ni kama vile Die tagseitung, Haneidelsbatt, Die Zeit, De tage speagal na mengineyo. Kwa ujumla, kutokana na dondoo na maelezo ya hapo juu yanadhihirisha kuwa lugha ya Kiswahili inalingana sana katika elimu na mawasiliano nje ya Afrika Mashariki,hivyo hali hii inapelekea lugha ya Kiswahili kupanda chati na hadhi kubwa zaidi ulimwenguni.

MAENEO YA WASWAHILI


Tuesday, 12 December 2017

Baadhiya Dhana za msingi kuhusu kiswhili

A) Kiswahili,
                    
                    Kiswahili lugha inayozungumzwa maeneo mbalimbali ya pwani ya Afrikaya mashariki pamoja na maeneo mengine mbalimbali ya Afrika.Lugha hii inamchanganyiko mkubwa wa msamiati kutoka lugha nyengine mbalimbali zilizokutana kimawasiliano na lugha hii.kama vile kiarabu,kihindi,kireno,kijerumani na kiengereza.

B)
    
      Waswhili,
             
                       Waswhili ni wenyeji wa mwambao wa afrika ya mashariki ambao lugha yao ya asili ni kiswahili,watu hawa na utamaduni wao wanajitafautisha na ule wa watu wengine katika baadhiya vipengele vya maisha,kama vile mavazi,malazi,malezi,dini na shughuli nyengine za  kiuhumi,

Uswahilini,
                     uswahilini ni eneo maalum la kijografia lililoanzia somalia upande wa kaskazini na kuishia upande wa kusini pamoja na visiwa vilivyomo katika eneo hilo la mwamao ya afrika ya mashariki.

D)

       Uswahili,
               
                         Ni utamaduni maalum wa waswahili unaoonekana katika matendo na maeneo ya waswahili wenyewe

TANBIHI:
                    Dhana ya mswahili,uswahili na uswahilini zimepotoshwa.kutoka uhalisia wake kuwa;

Mswahili:     ni mtu mdanganyifu,laghai namropokaji.

Uswahilini:   maeneo ya watu wajinga,ovyo,na wasio na mpangilio maalum wa hata ya makaazi yao.

Uswahili: Ni upuuzi, ujinga, ukale, unyama wa mawazo na maradhi ya kishirikina
                

Wednesday, 6 December 2017

nini maana ya mswahili?
 Assalamu alykum watanzania wenzangu.karibuni katika blogi yenu mpya anayohusu asili,uchanganuzi,na upambanuzi wa kiswahili cha mwambao na mswahili.
napenda kutoa changamoto .

je wakijuwa kiswahili cha mwambao?